Psalms 69:1-6

Kilio Cha Kuomba Msaada Wakati Wa Dhiki

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Yungiyungi. Zaburi ya Daudi)


1 aEe Mungu, niokoe,
kwa maana maji yamenifika shingoni.

2 bNinazama kwenye vilindi vya matope,
pasipo mahali pa kukanyaga,
Nimefika kwenye maji makuu,
mafuriko yamenigharikisha.

3 cNimechoka kwa kuomba msaada,
koo langu limekauka.
Macho yangu yanafifia,
nikimtafuta Mungu wangu.

4 dWale wanaonichukia bila sababu
ni wengi kuliko nywele za kichwa changu;
wengi ni adui kwangu bila sababu,
wale wanaotafuta kuniangamiza.
Ninalazimishwa kurudisha
kitu ambacho sikuiba.


5 eEe Mungu, wewe unajua upumbavu wangu,
wala hatia yangu haikufichika kwako.


6 Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
wakutumainio wasiaibishwe
kwa ajili yangu;
wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
Copyright information for SwhKC